Jumatano, 5 Machi 2014
MVUA KUBWA KUNYESHA KATIKA SAA 24 ZIJAZO
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania imetoa tahadhari kwamba mvua kubwa inayozidi milimita 50 inatarajiwa kunyesha ndani ya saa 24.
Maeneo yanayotarajiwa kupata mvua hizo ni ukanda wa Pwani yenye mikoa ya Mtwara, Lindi,Pwani, Dar es Salaam,Tanga pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.
Taarifa hiyo ya mamlaka ya hali ya hewa nchini imesema hali hiyo imetokana na kuimarika kwa mgandamizo mdogo wa hewa Mashariki mwa Bahari ya Hindi pamoja na kusogea kwa haraka kwa mfumo wa mvua za msimu, hivyo kuongeza kiwango cha unyevunyevu kutoka baharini kuelekea maeneo yaliyotajwa
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni