Wakili wa Oscar Pistorius leo ameamua
kuuponda ushahidi uliotolewa na wanandoa ambao walisema walisikia
mwanamke akipiga mayowe na kisha kusiki milio ya risasi usiku ambao
mwanariadha huyo alimuua mpenzi wake.
Wakili Barry Roux emesema kumekuwa na
uwiano wa ushahidi uliotolewa na wanandoa hao Michell Burger na mkewe
Charl Johnson, jambo ambalo linaonyesha walijiandaa kusema sawa ili
kupindisha ukweli.
Wakili huyo ameongeza kuwa kumekuwa
hakuna tofauti pia katika ushahidi walioutoa polisi baada ya tukio
hilo la kuuwawa kwa Reeva, jambo linaloashiria wanandoa hao walikuwa
wakifundishana watakachosema mahakamani.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni