.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 16 Aprili 2014

AJALI YA KIVUKO HUKO HUKO KOREA KUSINI, VIFO VYAONGEZEKA HADI KUFIKIA WATU 4, 164 WAOKOLEWA NA 300 BADO HAWAJAPATIKANA

 Mamia ya boti, helkopta za uokoaji na wazamiaji wameendelea na harakati za uokoaji wa mamia ya abiria waliokuwa katika kivuko kilichokuwa na abiria 470 kilichozama huko Korea Kusini. 

Tayari watu 164 wameokolewa huku taarifa zikisema watu 4 wamefariki dunia katika ajali hiyo.
 Kati ya waliofariki ni pamoja mwanamke mwenye miaka 27 aliyetambulika kwa jina la Park Ji-Yeong na mwanafunzi Jeong Cha Woong. 

Mpaka sasa zaidi ya abiria 300 ambao wengi wao ni wanafunzi waliokuwa wanasafari na kivuko hicho bado hawajaokolewa na juhudi za kuwatafuta zinaendelea kwa kasi kubwa. Walikuwa wanaelekea katika kisiwa cha kusini cha Jeju
       Sehemu ya kivuko hicho inavyoonekana wakati ikiendelea kuzama baharini
 Mamia ya boti za uokoaji zikijumuisha za wavuvi zikielekea kilipo kivuko hicho tayari kutoa msaada wa waathirika
Mmoja wa walionusurika katika ajali hiyo akiokolewa kwa kutumia helkopta

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni