Afisa Habari wa Bunge Bw. Prosper Minja akitoa maelezo mbele ya Makamu wa Rais wa Tanzania Mhe, Dkt. Gharib Bilal (katikati) juu ya kazi mbalimbali zifanywazo na Ofisi ya Bunge wakati alipotembelea Banda la Bunge leo kwenye Maadhimisho ya kuelekea Miaka Hamsini ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Elisante Ole Gabriel na kulia ni Mhe. Mohamed Aboud
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) Bw. Asangye Bangu akitoa maelezo ya kina mbele ya Makamu wa Rais wa Tanzania Mhe, Dkt. Gharib Bilal (katikati) kuhusu namna Bodi hiyo inavyofanya kazi katika kutoa mikopo kwa wanafunzi mbalimbali nchini mara alipotembelea Banda la Bodi ya Mikopo leo kwenye Maadhimisho ya kuelekea Miaka Hamsini ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Elisante Ole Gabriel
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni