Mabaki ya ndege ya Algeria
iliyotoweka ikiwa na abiria 116 wakati ikitokea Burkina Faso kwenda
Algiers yamepatikana nchini Mali.
Rais wa Ufaransa ambaye nchi yake
ilikuwa na abiria 51 kwenye ndege hiyo amesema ametuma kikosi chake
kwenda katika eneo ilipoanguka ndege hiyo.
Kituo cha kuongozea ndege kilipoteza
mawasiliana na ndege hiyo mali ya Swiftair hapo jana baada ya rubani
kutoa taarifa ya kuwepo kwa mvua kubwa.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni