.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 28 Julai 2014

RAIS JK ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA ALHAJI R. KUNDYA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametuma salamu za rambirambi kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mheshimiwa Dkt. Parseko V. Ole Kone kuomboleza kifo cha aliyepata kuwa Naibu Waziri, Mbunge na Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), Mheshimiwa Alhaji Mahami Rajab Kundya.

Mzee Kundya aliaga dunia jana, Jumapili, Julai 27, 2014 mjini Zanzibar.

Katika salamu zake, Rais Kikwete amesema kuwa ni jambo la kusikitisha kuwa taifa limempoteza Mzee Kundya katika kipindi ambacho ushauri wake ulikuwa unahitajika sana na kuwa Watanzania wataendelea kumkumbuka kwa mchango wake katika nafasi zote alizozishikilia za Serikali, za Chama cha Mapinduzi na za kidini.

Naungana nawe na wana-Singida wote katika kuomboleza kifo cha Mzee Kundya.Tumepoteza kiongozi ambaye mchango wake utaendelea kukumbukwa na sisi sote. Kupitia kwako, natuma pia salamu zangu za rambirambi kwa familia ya marehemu.

Niko nao katika kuomboleza msiba huu mkubwa na naungana nao katika kumwomba Mwenyezi Mungu aiweke peponi roho ya Marehemu Mzee Kundya,” amesema Rais Kikwete.

Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
28 Julai,2014

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni