.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 6 Agosti 2014

BRITISH AIRWAYS YASITISHA SAFARI ZAKE ZOTE KUELEKEA SIERRA LEONE NA LIBERIA

 Shirika la ndege la Uingereza, British Airways limesitisha safari zake zote za ndege kuelekea mji mkuu wa Sierra Leone, Freetown pamoja na mji mkuu wa Liberia, Monrovia hadi hapo tarehe 31 mwezi huu wa nane. 

Taarifa ya shirika hilo iliyotolewa na msemaji wake imesema kuwa, kufutwa kwa safari hizo ni kutoka na nchi hizo hivi sasa kukumbwa na ugonjwa wa Ebola.

Msemaji huyo amesema kusitishwa kwa safari hizo ni kwa ajili ya kulinda usalama wa abiria wao, wahudumu wa ndege pamoja na wafanyakazi wote wa shirika hilo.
Tayari ugonjwa huo wa Ebola umeshaua watu wapatao 880 katika nchi za Afrika Magharibi 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni