Kocha Louis van Gaal ametwaa kikombe
chake cha kwanza akiwa na Manchester United, baada ya kuifunga
Liverpool kwa mbao 3-1 na kubeba Kombe la Kimataifa la Mabingwa.
Mabao ya Manchester United yalitiwa
kimiani na Wayne Rooney, Juan Mata pamoja na kinda Jesse Lingard
huku Liverpool wakipata bao lao la kufutia machozi kupitia kwa Steve
Gerrard.
Kwa ushindi huo Manchester United
itakwea pipa Marekani kurejea nyumbani Uingereza baada ya kucheza
michezo mitano nchini humo, bila ya kufungwa hata mchezo mmoja.
Wayne Rooney akishangilia goli lake
Wachezaji wa Manchester United wakimpongeza Mata baada ya kufunga bao



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni