Mmoja wa wauaji wa kulipwa hatari
nchini Colombia ameachiwa huru kutoka gerezani baada ya kutumikia
kifungo cha miaka 22 jela kati ya miaka 30 aliyoadhibiwa.
Muuaji huyo John Jairo Velasquez,
aliyepewa jina la utani la Popeye, alikuwa ni mdunguaji mzuri wa
kutumia silaha wa mfanyabiashara mkubwa wa dawa za kulevya Pablo
Escobar.
Valasquez alikiri kuua watu 300 na
pia kukiri kushiriki katika kufanikisha mauaji ya watu 3,000 katika
miaka ya 1980 na 1990.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni