Muigizaji nguli wa filamu nchini
Marekani Robin Williams amekutwa amekufa nyumbani kwake katika tukio
ambalo linaaminika kuwa ni la kujiua.
Polisi wa Kaunti ya Marin
wamethibitisha kifo cha muigizaji huyo nyota mwenye umri wa miaka 63,
baada ya maafisa wa msaada wa dharura kufika nyumbani kwake jana
mchana.
Williams alikuwa ni maarufu katika
uigizaji kwenye filamu kama Good Morning Vietnam na Dead Poets
Society na alishinda tuzo za Oscar kwa uhusika wake kwenye filamu ya
Good Will Hunting.
Katika salamu zake za rambirambi
Rais Barack Obama amesema Williams aliwafanya watu wacheke na
aliwafanya watu walie katika uigizaji wake wakati wa uhai wake.
Mtoto akiweka maua mbele ya nyumba ya Robin Williams



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni