Baada ya wiki iliyopita nyumba ya
Mfalme wa Pop marehemu Michael Jackson kuwekwa sokoni nyumba nyingine
ya mkali huyo wa Pop iliyopo Las Vegas imewekwa sokoni kwa bei ya
dola milioni 19.5.
Nyumba hiyo aliishi Michael Jackson
mnamo mwaka 2006 hadi 2008 aliporejea Marekani akitokea Bahrain
ambapo alienda kujihifadhi baada ya kutokutwa na hatia ya
kuwadhalilisha watoto.
Nyumba hiyo ina vyumba 12 ikiwa na
sehemu ya chini ya ardhi inaukubwa wa futi mraba 7,394, pamoja na
eneo la kukutana na wageni lenye uwezo wa kukaa watu 74.



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni