Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel amewasili katika mji mkuu wa Ukraine, Kiev tayari kwa mazungumzo na rais wa nchi hiyo, Petro Poroshenko.
Kiongozi huyo ameonyesha kuiunga mkono Ukraine kufuatia mzozo unaondelea nchini humo na waasi wanaoungwa mkono na Urusi.
Wakati Kansela Merkel akiwa na mazungumzo na rais wa Ukraine, malori yaliyokuwa yamebeba misaada toka Urusi yamegeuza na misaada hiyo kurejea Urusi.
Zaidi ya malori 200 yameondoka mashariki mwa mji wa Luhansk ambao unadhibitiwa na waasi wanaoipinga serikali ya Ukraine.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni