.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 23 Septemba 2014

DKT. SHEIN AONGOZA MAMIA YA WAOMBOLEZAJI KWENYE MAZISHI YA MAREHEMU IDDI PANDU HASSAN, ZANZIBAR

Marehemu Iddi Pandu Hassan aliyekua Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (wa nnne kulia) akiwepo na Rais Mstaafu wa Zanzibar DK.Amani Abeid Karume wakijumuika na waisalmu katika kumswalia Marehemu aliyekua Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Iddi Pandu Hassan katika Msikiti wa Mchekeni Magomeni Mjini Zanzibar leo na Kuzikwa kijijini kwao Makunduchi.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein na Makamo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ALhaj Dk. Mohamed Gharib Bilali waliungana na wananchi mbali mbali katika maziko ya aliyekua Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Iddi Pandu Hassan aliyezikwa kijijini kwao Kipunguni Makunduchi jana.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein alipofika nyumbani kwa Marehemu Iddi Pandu Hassan aliyekua Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwapa pole wafiwa leo kabla ya kufanyika mazishi huko kijijini kwao Makunduchi.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Ndugu wa Marehemu Iddi Pandu Hassan aliyekua Mwanasheria Mkuu wa Serikali alipofika kuwapa pole wafiwa nyumbani kwa marehemu Magomeni Mjini Zanzibar leo kabla ya kufanyika mazishi huko kijijini kwao Makunduchi.

Baadhi ya akina mama walioshiriki katika mazishi ya aliyekua Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Marehemu Iddi Pandu Hassannyumbani kwake Magomeni Mjini Unguja jana.{Picha na Ramadhan Othman Ikulu.]

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni