.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 30 Septemba 2014

IDADI YA WATU WALIOFIKISHWA HOSPITALI WAKIWA NA HALI MBAYA KWA KUNYWA TOGWA MJINI SONGEA YAONGEZEKA

Baadhi ya wagonjwa waliolazwa katika hospitali ya Peramiho mkoani Ruvuma baada ya kunywa pombe aina ya Togwa inayosadikiwa kuwa na sumu. 

Idadi ya watu waliofikishwa hospitali mjini Songea mkoani Ruvuma kutokana na kunywa pombe aina ya Togwa inayosadikiwa kuwa na sumu sasa imefikia 325. 

Taarifa toka mkoani humo zinasema kuwa, idadi hiyo imeongezeka leo kutokana na wagonjwa zaidi wanaoharisha na kutapika kufikishwa katika hospitali ya misheni Peramiho na zahanati ya Lyangweni na baadhi yao wakiwa na hali mbaya. 

Watu hao walikumbwa na mkasa huo wakiwa katika sherehe ya kipaimara iliyoandaliwa na mkazi mmoja wa mjini Songea.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni