Timu ya soka ya FC Barcelona imeibuka na ushindi mnono wa mabao 5-0 dhidi ya wenyeji wao Levante katika mchezo wa ligi kuu nchini Hispania " La Liga ".
Katika mchezo huo ulionekana kutawaliwa zaidi na Barcelona, mchezaji mahiri ulimwenguni Lionel Messi alikosa penati lakini baadaye alirekebisha makosa kwa kufunga bao safi.
Mabao ya Barcelona yaliwekwa kimiani na wachezaji Neymar akifunga bao la kwanza kisha Ivan Rakitic akafunga mabao mawili kabla ya mapumziko.
Baada ya kuanza kwa kipindi cha pili, Sandro akaifungia Barcelona bao la tatu kabla ya Lionel Messi kukosa penati lakini akaja kufunga bao la nne na bao la tano likawekwa kimiani na Pedro.
Lionel Messi akiwa katikati ya mabeki wa Levante
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni