Mario Balotel ameonyesha kiwango chake na kiu ya kufumania nyavu baada ya usiku wa kuamkia leo kufunga bao moja kati ya mabao 2-1 waliyopata Liverpool dhidi ya wageni wao Ludogorets katika mchezo wa ligi ya mabingwa barani Ulaya uliochezwa Anfield.
Mtukutu Balloteli alifunga bao la kwanza katika dakika ya 81 kabla ya nahodha Steven Gerald ahajafunga bao la pili kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 90.
Bao pekee la Ludogorests lilifungwa na Dani Abalo pia katika muda wa majeruhi wa mchezo huo.
Mlinda mlango wa Ludogorets, Borjan akiruka bila mafanikoo kuokoa mpira ulipigwa na Mario Balloteli ambao ulizama kimiani na kuiandikia Liverpool bao la kwanza.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni