Mchezaji Nyota Mkongwe wa Argentina Gabriel Batistuta anadaiwa kumuomba daktari wake amkate miguu yake ili kumuepusha na maumivu makali aliyonayo tangu astaafu soka mnamo mwaka 2005.
Mshambuliaji huyo ambaye alicheka na
nyavu mara 56 kati ya mechi 78 katika michuano ya kimataifa,
anasumbuliwa mno na maumivu ya miguu kutokana na mikiki mikiki
aliyokuwa akifanya dimbani katika kipindi cha miaka 17 ya soka.
Batistuta kwa sasa hawezi kutembea
na hulazimika kujisaidia haja ndogo akiwa kitandani kutokana na
kushindwa kabisa kunyanyuka na kutembea kwa kutumia miguu yake iliyo
na maumivu makali.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni