Kituo cha Televisheni ya Taifa cha
Pakistani kimerejesha matangazo yake tena hewani baada ya vikosi vya
usalama kuwaondoa waandamanaji wanaoipinga serikali kutoka katika
makao makuu ya kituo hicho Jijini Islamabad.
Vikosi vimetumwa katika kuwadhibiti
waandamanaji wasikitwae kituo hicho baada ya kuingia katika ofisi
hizo za PTV.
Waandamanaji hao watiifu kwa
kiongozi wa upinzani Imran Khan na kiongozi wa kidini Tahirul Qadri
wanataka Waziri Mkuu Nawaz Sharif kujiuzulu kwa tuhuma za rushwa na
wizi wa kura.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni