Mkurugenzi wa Lino International Agency ambao ni Waandaaji
wa mashindano ya Urembo ya Miss Tanzania,Hashim Lundenga akionyesha nakala ya
cheti cha kuzaliwa cha Mrembo Sitti Mtemvu alicholetewa na wakazazi wake.
Mkurugenzi wa Lino International Agency ambao ni Waandaaji
wa mashindano ya Urembo ya Miss Tanzania,Hashim Lundenga (kati) akiongea na
waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya sakata la umri halali wa Mrembo
alietwaa taji hilo Mwaka huu, Sitti Abbas Mtemvu (kushoto),katika mkutano huo
Lundenga alitolea ufafanuzi swala la umri wa Mrembo huyo kulingana na vilelezo
alivyopewa na mrembo huyo wakati akijiunga na mashindano hayo
Lundenga aliendelea kusema kuwa Mashindano ya Miss Tanzania
hayaruhusu mshiriki yeyote mwenye mtoto kushiri,hivyo katika swala la Sitti
Mtemvu kuwa ana mtoto,hilo kalina ukweli wowote bali ni uvumi tu wa kwenye
mitandao ya kijamii baada ya Mrembo huyo kuonekana akiwa katika picha na mtoto
aliyeomba kupiga nae.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni