Mwanariadha mlemavu Oscar Pistorius raia wa Afrika Kusini amehukumiwa kwenda gerezani miaka mitano ( 5 ) baada ya mahakama kumtia hatiani kwa kosa la kumuua mpenzi wake, mwanamitindo Reeva Steenkamp kwa kumpiga risasi, tukio ambalo lilitokea siku ya wapendanao ( valentine day ) mwaka jana.
Hukumu hiyo ilianza kusomwa asubuhi na kuvuta hisia mbalimbali toka kwa waliokuwa wanaifuatilia kesi hiyo.
Jaji Masipa alisema kabla ya kutoa hukumu hiyo, changamoto kubwa iliyokuwa inamkabili ni kupata adhabu ambayo itaridhisha pande zote mbili katika kesi hyo.
Mwanariadha Oscar Pistorius akitolewa mahakamani chini ya ulinzi mkali wa polisi.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni