Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe
(kushoto) akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Regina Chonjo
mabati 2000 kwa ajili ya ujenzi wa Maabara za Shule 20 za Sekondari
wilayani humo. Waziri Chikawe ametoa msaada huo baada ya Rais Jakaya
Kikwete kutoa agizo kwa kila mwana jamii nchini kuchangia ujenzi wa
maabara katika shule za Kata nchini. Picha na Felix Mwagara.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (wapili
kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Regina Chonjo, Mwenyekiti wa
Halmashauri ya Wilaya hiyo, Abdalla Chikawe (wapili kulia) na
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Valery Kwembe
wakiyaangalia msaada wa mabati yaliyotolewa na Mbunge wa Jimbo hilo
kwa ajili ya kuzisaidia Shule za Sekondari za Kata kwa ajili ya
ujenzi wa maabara. Makabidhiano ya mabati hayo 2000 yalifanyika
nyumbani kwa Waziri Chikawe mjini Nachingwea leo. Picha zote na Felix
Mwagara.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni