.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 29 Novemba 2014

BOKO HARAMU WAHUSISHWA ULIPUAJI WA MSIKITI MJINI KANO AMBAPO WATU 120 INASADIKIWA KUFARIKI DUNIA

Inasadikiwa kuwa zaidi ya waumini 120 wamefariki dunia na wengine zaidi ya 270 wamejeruhiwa baada ya kutokea milipuko ya mabomu wakati wakiwa katika ibada ya ijumaa katika msikiti mkuu wa Grand uliopo mjini Kano nchini Nigeria jana mchana.
Mabamu matatu yanasemekana kulipuliwa katika msikiti huo, na bomu la kwanza lililipuka wakati mshambuliaji alipokuwa anataka kuingia na gari ndani ya maegesho ya magari ya msikiti huo. 

Wapiganaji wa kundi la Boko Haramu wanahusishwa na tukio hilo la kuhuzinisha.
Kundi la Boko Haramu limekuwa likifanya vitendo vya utekaji na mauaji ya mara kwa mara katika maeneo mbalimbali nchini Nigeria.
Moshi mkubwa ukionekana kutanda katika eneo la msikiti huo huku wananchi wakishuhudia.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni