Wakicheza nyumbani, Crystal Palace baada ya kufungwa bao hilo walijpanga na kuanzisha mashambulizi ya mara kwa mara langoni mwa Liverpool.
Mashambulizi hayo yalizaa mabao kupitia kwa Dwight Gayle aliyefunga bao la kusawazisha katika dakika ya 17, bao la pili likifungwa na Ledley katika dakika ya 78 na bao la 3 nala ushindi likifungwa na Mile Jedinak kunako dakika ya 81.
Mambo magumu msimu huu hadi namkumbuka Suarez!! Kocha wa Liverpool, Brendan Rodgers akiwa mnyonge baada ya timu yake kuchapwa 3-1.
Hata mimi kiduku nakiweza!! Kocha wa Crystal Palace, Neil Warnock akifurahia matokeo hayo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni