Ndege ya shirika la ndege la Flybe ikiwa na abiria 63 imelazimika kutua kwa dharura katika uwanja wa ndege wa Belfast baada ya kuwepo kwa harufu ya moshi kutoka katika sehemu ya kubeba mizigo ya ndege hiyo.
Ndege hiyo namba BE990 iliyokuwa inatokea Southampton ilitua salama na tayari magari ya zimamoto na kubeba wagonjwa yalikuwa yameandaliwa uwanjani hapo tayari kutoa msaada wowote ambao ungehitajika.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni