Mratibu wa tuzo za uongozi bora wa bodi katika sekta za
benki na bima,Bi Neema Gerald (wa pili kulia) akiongea na waandishi wa habari
(hawapo pichani) katika mkutano na vyombo vya habari uliofanyika jijini Dar es Salaam
jana, kutangaza uzinduzi wa tuzo za uongozi bora wa bodi katika sekta za benki
na bima, ambazo zitamulika na kutambua mchango wa uongozi uliotukuka wa bodi za
wakurugenzi kwenye sekta za benki na bima nchini. Tuzo hizo zimepangwa
kufanyika jijini Dar es Salaam January 30, 2015. Ameambatana na Bw. Laurence
Mwangoka (wa kwanza kulia), Meneja Mauzo wa Serena Hotel ambao ni moja ya
wadhamini wa tuzo hizo pamoja na wawakilishi kutoka Capital Plus International
(CPI), Bw. Matthew Kasonta (wa pili kushoto), na Bw. Kassim Malela (kushoto)
Bw. Matthew Kasonta (katikati), mwakilishi kutoka Capital
Plus International (CPI) ambao ni moja ya wadhamini wa tuzo za uongozi bora wa
bodi katika sekta za benki na bima akiongea na waandishi wa habari (hawapo
pichani) katika mkutano na vyombo vya habari uliofanyika jijini Dar es Salaam
jana, kutangaza uzinduzi wa tuzo za uongozi bora wa bodi katika sekta za benki
na bima, ambazo zitamulika na kutambua mchango wa uongozi uliotukuka wa bodi za
wakurugenzi kwenye sekta za benki na bima nchini. Tuzo hizo zimepangwa
kufanyika jijini Dar es Salaam January 30, 2015. Ameambatana na Bw. Laurence
Mwangoka (wa kwanza kulia), Meneja Mauzo wa Serena Hotel ambao ni moja kati ya
wadhamini wa tuzo, Mratibu wa tuzo hizo, Bi. Neema Gerald (wa pili kulia) na
mwakilishi kutoka Capital Plus International (CPI) Bw. Kassim Malela
(kushoto).
TUZO za Bodi yenye Uongozi Bora ijulikanayo kama Best Board
Leadership Award (BBLA), ambazo zimelenga kutambua uongozi bora wa Bodi za Wagurugenzi
katika sekta ya kibenki na bima, zimepangwa kufanyika jijini Dar es Salaam
mwishoni mwa mwezi ujao. BBLA iliyopangwa kufanyika mwezi Januari tarehe 30 na kufanyika
kwa mara ya kwanza nchini, inaandaliwa chini ya mwamvuli wa Chama cha Mabenki
Tanzania (TBA) na Chama cha Makampuni ya Bima Tanzania (ATI).
Akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar
es Salaam jana, Mratibu wa BBLA Bi. Neema Gerald alisema tuzo hizo zinatoa
fursa ya ufahamu wa jinsi gani bodi bora inaweza kusaidia taasisi kupata
mafanikio na kufikia utendaji bora hususani katika eneo walilobobea kiutalaam.
Wadhamini wa tukio hilo la kipekee ni pamoja na Capital Plus
Internaional Limited, Real PR Solutions Limited, Afrimax Strategic Partnerships
Limited, Serena Hotel na IPP Media, wakati wadhamini wengine wakiaswa
kujitokeza zaidi kuunga mkono tuzo hizo.
"Tumeona umuhimu wa kutambua na kuthamini mchango
unaotolewa na wakurugenzi wa bodi katika taasisi zao.Tunaamini kuwa katika kila
mafanikio ya taasisi ya kifedha, nyuma yake kuna bodi ya wakurugenzi imara na
makini. Sasa, sifa hizo ambazo wajumbe wa bodi wengi wanakuwazo zinapaswa
kutambuliwa na kuthaminiwa, "alisema.
Bi. Neema alisema kuwa utamaduni unaojulikana ni kuwa ni
Maafisa Watendaji Wakuu na Wakurugenzi Wakuu pekee ndiyo wanaothaminiwa na kutambuliwa
na waajiriwa au jamii nzima kwa ujumla.
"Ni wakati muafaka sasa kwa bodi
zenye utendaji bora kutambuliwa na kuzawadiwa kikamilifu kwa jitihada
zao," alisema. Alibainisha kuwa zoezi hilo, tathmini na upangaji wa mwisho
wa matokeo utafanywa na jopo la majaji waliobobea na wenye rekodi bora za
kiutendaji.
Tathmini hiyo italenga zaidi katika ufanisi wa Bodi ya Wakurugenzi
katika suala la utawala wa taasisi, usimamizi wa fedha na uwezo wa kuiongoza
dira ya taasisi kwa ujumla wake. Maeneo mengine ni umakini wa bodi katika
uwazi, uwajibikaji, utendaji, na ufuataji wa hatua madhubuti na utendaji wake.
Alitaja maeneo mengine ambayo bodi itafanyiwa tathmini kuwa
ni utoaji wa mitazamo yakinifu ya bodi katika kusisitiza umuhimu wa utendaji wa
mtaji watu katika ngazi ya bodi na kuweka mbele vigezo vitakavyowezesha utendaji
bora zaidi wa bodi, "alisema.
Aliongeza kuwa tuzo hizo zimeanzishwa kwa wakati muafaka nchini
wakati ambapo sekta za Bima na kibenki zinapitia mabadiliko makubwa na
kujitokeza kwa makampuni mengi ya bima na masoko zaidi kuongezeka ili kufikia
wateja wengi katika nyanja zote za maisha.
"Kwa mabadiliko haya wakati huu, hasa katika sekta ya
fedha ambapo idadi kubwa ya makampuni ya bima na mabenki zimekuwa zikifungua biashara
Tanzania, wateja wanahitaji kuwa na uhakika kuwa malipo yao ya bima yako salama
na wanaweza kupatiwa kwa wakati wowote", alisema, na kuongeza:
"Hili litafanikiwa tu endapo kampuni hiyo ya bima au
benki itaendelea kufanya kazi kwa mafanikio. Kwa maana hiyo, bodi ya wakurugenzi
itakuwa na jukumu muhimu katika kuhakikisha kampuni hiyo haifi, "alisema.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni