Timu ya soka ya Chelsea imezindukia katika kombe la FA baada ya kuitandika Watford mabao 3-0 katika mchezo uliochezwa uwanja wa Stamford Bridge.
Chelsea ambayo juzi ilipata kipigo cha aina yake cha mabao 5-3 toka kwa Tottenham katika mchezo wa ligi kuu Uingereza, jana ilipata ushindi huo katika mchezo wa FA kwa mabao yaliyowekwa kimiani na William, Loic Remy na Kurt Zouma na kuifanya Chelsea kusonga mbela katika michuano hiyo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni