Fidel Odinga ambaye ni mtoto wa
kiongozi wa muungano wa CORD nchini Kenya Raila Odinga, amekutwa
akiwa amekufa leo asubuhi nyumbani kwake eneo la Karen.
Mwili wa mtoto huyo wa Raila Odinga,
umekutwa ukiwa kitandani kwake, na kuchukuliwa kwenda kuhifadhiwa Lee
Funeral Home.
Polisi Jijini Nairobi wamesema bado
haijafahamika ni nini kilichopelekea kutokea kwa kifo hicho.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni