Shahidi amedai kuwa Naibu Rais wa
Kenya William Ruto aliichochea jamii ya kabila la Kalenjin kuwauwa
watu wa kabila la Kikuyu katika machafuko yaliyotokea kwenye uchaguzi
wa mwaka 2007.
Shahidi huyo ameiambia mahakama ya
Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita (ICC), kuwa Ruto aliwachochea
wakalenji kuwafukuza wakikuyu katika mkoa wa Bonde la Ufa, iwapo
chama chake ODM hakitashinda uchaguzi wa mwaka 2007.
Hata hivyo wakili wa Ruto, alipinga
madai hayo na kusema ni ya uongo na yaliyotungwa dhidi ya mteja wake.
Ruto na mtangazaji Joshua arap Sang wanakabiliwa na kesi ya uhalifu
dhidi ya binadamu walioutenda wakati wa ghasia za uchaguzi za mwaka
2007-2008.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni