.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 11 Januari 2015

ZIARA YA NAIBU WAZIRI WA MAJI, MH MAKALLA JIJINI MBEYA

Eng Martin Kimambo akimwonyesha na kumpa maelezo Naibu Waziri wa Maji, Mh Amos Makalla kuhusu miundombinu ya maji taka eneo la Kalobe.
Naibu Waziri wa Maji, Mh Makalla akiangalia chujio la maji eneo la Swaya.
Naibu Waziri wa Maji, Mh Amos Makalla kishuka kutoka tanki la Kadege.
Naibu Waziri wa Maji, Mh Amos Makalla akikagua chanzo cha chemchem Nzovwe.
Naibu Waziri wa Maji, Mh Amos Makalla akimsiliza mwenyekiti wa bodi ya maji Jaji Atuganile Ngwale.

Naibu Waziri wa Maji, Mh Amos Makalla akiongea na bodi na menejimenti ya mamlaka maji jiji la Mbeya baada ya Naibu waziri huyo kutembelea mamlaka ya maji safi jijini Mbeya. Aidha aliipongeza mamlaka hiyo kwa kuongeza wateja kutoka 9000 mwaka 2002 na kufikia 40,000. 

Mh Makall pia aliipongeza kwa kuwa mamlaka ya tatu kitaifa kuwa na miundombinu ya majita, huku pia akiiagiza kudhibiti upotevu wa maji kutoka asilimia 34 ya sasa na wafikie kiwango cha kimataifa asilimia 20. 

Mh Makalla amezitaka mamlaka zingine kushirikiana na mamlaka kutokutoa vibali vya makazi eneo la vyanzo vya maji na pia amewataka wananchi kutunza, kutolima, kukata miti na kuchafua vyanzo vya maji

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni