Zoezi la kutafuta kisanduku cha
kurekodi taarifa cha ndege ya abiria iliyoanguka ya AirAsia, limeanza
wakati hali ya hewa ikianza kuboreka katika bahari ya Java.
Ndege hiyo namba QZ8501 ilikuwa
ikitokea Surabaya, Indonesia kwenda Singapore Desemba 28, ikiwa na
abiria 162 kabla ya kutoweka kwenye rada.
Msako umefanikiwa kupata miili 37
hata hivyo mabaki ya miili ya wahanga wa ajali hiyo inaaminika kuwa
bado ipo ndani ya ndege chini ya bahari.
Hali mbaya ya hewa imekwamisha
jitihada za wazamiaji kufikia kitu kimoja kikubwa kinachohisiwa kuwa
ni mabaki ya ndege hiyo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni