Mvutano baina ya Marekani na Israel
umeongezeka, baada ya Waziri Mkuu wa Israel Benjamin
Netanyahukuituhuma Marekani na mataifa mengine kushindwa kuizuia Iran
kumiliki silaha za nyuklia.
Kufuatia kauli hiyo Wizara ya Mambo
ya Nje ya Marekani, imemuhoji Bw. Netanyahu kuhusina na matamshi hayo
ya kuituhumu Marekani.
Wakati hayo yakiendelea viongozi wa
chama cha Republican, wamemualika Bw. Netanyahu, kuhutubia baraza la
Congress la Marekani wiki ijayo, jambo ambalo limekikasirisha chama
cha Democrats.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni