Rais wa Namibia anayeondoka
madarakani Hifikepunye Pohamba ameshinda tuzo yenye thamani kubwa ya
Mo Ibrahim inayotolewa kwa viongozi wa bara la Afrika.
Tuzo hiyo ya dola milioni 5,
hutolewa kila mwaka kwa kiongozi wa nchi wa kuchaguliwa aliyeongoza
vyema taifa lake na kuboresha masha ya watu wake na kisha kuondoka
madarakani.
Hata hivyo tuzo za miaka iliyopita
kwa mara nne katika kipindi cha miaka mitano zilishindwa kupata
mshindi.
Bw. Pohamba, ambaye alikuwa ni muasi
aliyepigania uhuru wa nchi yake, ametumikia taifa lake katika nafasi
ya urais kwa vipindi vya mihula miwili.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni