.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 26 Machi 2015

TAARIFA ZASEMA RUBANI MWENZA WA NDEGE YA GERMANWINGS ALIIANGUSHA KWA MAKUSUDI

Maafisa wameeleza kuwa rubani mwenza wa ndege ya shirika la Germanwings iliyoanguka kwenye Mlima Alps, aliyejulikana kama Andreas Lubitz, inawezeka alikuwa anataka kuiteketeza ndege hiyo.

Mwendesha mashtaka wa Marseille, Brice Robin, kwa kutumia sauti zilizorekodiwa na sanduku la kurekodi taarifa la "black box", amesema rubani huyo alikuwa akiongoza ndege peke yake.

Amesema kuwa rubani huyo aliishusha ndege chini kwa makusudi, huku rubani mwenzake akiwa amefungiwa nje ya chumba cha kuongozea ndege.

Bw. Robin amesema rubani Lubitz alikuwa kimya kabisa wakati rubani mwenzake akihangaika kuingia kwenye chumba cha kuongozea ndege.
                                            Polisi wakiilinda nyumba ya rubani Lubitz

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni