.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 1 Aprili 2015

KUTOKA BUNGENI MJINI DODOMA HII LEO

1
Naibu Waziri Wizara Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto Mhe.Pindi Chana akijibu swali la msingi la Mhe.Kidawa Salehe (Mb) Viti Maalum CCM lililohoji juu ya Serikali imefanya utafiti gani juu ya sababu za ukatili kwa watoto,bungeni Mjini Dodoma 1 Aprili,2015.
2
Naibu Waziri Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Mhe.Stephen Kebwe akijibu swali la Mhe.Maryam Msabaha (Mb) Viti Maalum CHADEMA lililohusu serikali inamikakati gani kuboresha Hospitali zetu wananchi wa vijijini waweze kupata huduma hiyo kiurasi,Bungeni Mjini Dodoma.
3
Naibu Waziri wa Nchi,Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Mhe.Stephen Masele akijibu swali la Msingi la Mhe.Amina Makilagi (Mb) Viti Maalum CCM lililohoji kuhusu serikali itatumia lini tafiti zilizofanyika zakutumia nishati Mbadala, Bungeni Mjini Dodoma 1 Aprili,2015 .
4
Naibu Waziri Wizara ya Nishati na Madini Mhe.Charles Mwijage akijibu swali la Msingi la Mhe.Moses Machali (Kasulu Mjini) lililohoji kuhusu utekelezaji wa mradi wa umeme kutoka Mto Malagarasi ambao ulipaswa kutekelezwa kwa kutumia fedha za MCC Bungeni Mjini Dodoma 1 Aprili,2015.
5
Mbunge wa Kisarawe (CCM) Mhe.Seleman Jafo akiwasilisha hoja binafsi kuomba tarehe ya kura ya maoni isogezwe mbele na kupendekeza Serikali ipeleke Muswada Bungeni wa hati ya dharura kupitisha Katiba ya mpito,Bungeni Mjini Dodoma 1 Aprili,2015 .
6
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akitoka nje ya ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma mara baada ya kuhairisha bunge kutokana na fujo zilizozuka ndani ya bunge kutoka na kuwepo kwa mwingiliano wa hoja binafsi kati ya Mhe.Seleman Jafo (Mb) CCM Kisarawe na Mhe.John Mnyika (Mb)Ubungo CHADEMA Bungeni Mjini Dodoma 1 Aprili,2015.
7
Baadhi ya wabunge wakiwa nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma mara baada ya Spika kuhairisha bunge kutokana na kuzuka kwa fujo Bungeni Mjini Dodoma 1 Aprili,2015. 

                                                          Picha na Anitha Jonas – MAELEZO,Dodoma

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni