.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 4 Aprili 2015

LIGI KUU UINGEREZA, KIVUMBI LEO NI ARSENAL NA LIVERPOOL

Kivumbi cha ligi kuu nchini Uingereza kitaendelea hii leo katika viwanja mbalimbali, lakini mchezo unaosubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa soka ni mchezo kati ya washika bunduki wa jiji la London, Arsenal ambao watakaokuwa nyumbani katika uwanja wao wa Emirates kucheza na Liverpool. 

Arsenal wana pointi 60 wakiwa katika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi hiyo huku Liverpool wakiwa katika nafasi ya tano wakiwa na pointi 54.

Liverpool wanashuka dimbani wakiwa na kumbukumbu ya kufungwa mabao 2-1 na Manchester United mchezo uliochezwa March 22’ 2015 Anfield, wakati Arsenal wao waliwatandika Newcastle 2-1 mchezo uliochezwa March 21’2015.

Mchezo mwingine ni kati ya vinara wa ligi hiyo Chelsea ambao watakuwa nyumbani darajani kucheza na Stoke City.

Mechi nyingine hii leo ni kama ifuatavyo:-

Everton vs Southampton

Leicester vs West Ham

Manchester United vs Aston Villa

Swansea vs Hull

West Brom vs QPR

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni