.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 29 Aprili 2015

LIGI KUU UINGEREZA, LIVERPOOL HOI KWA HULL CITY

Mshambuliaji wa Hull City Michael Dawson akiwa ameruka juu na kuupiga kichwa mpira uliomshinda mlinda mlango wa Liverpool, Simon Mignolet na kujaa moja kwa moja wavuni.
Timu ya soka ya Liverpool imeendelea kujiweka pabaya kushindwa kuingia nne bora, baada ya jana usiku kukubali kipigo cha bao 1-0 toka kwa Hull City katika mchezo wa ligi kuu nchini Uingereza. 

Katika mchezo huo, bao la wenyeji lilifungwa na Michael Dawson kwa kichwa kunako dakika ya 37 ya kipindi cha kwanza. 

Kwa matokeo hayo Liverpool wamesimama katika nafasi ya tano wakiwa na jumla ya pointi 58 huku Hull wakiwa katika nafasi ya 15 wakiwa na pointi 34.







Hakuna maoni :

Chapisha Maoni