Wachezaji wa timu ya soka ya Juventus ( bibi kizee cha Turini ) ya Italia wakishangilia kufuzu kwa hatua ya nusu fainali ya ligi ya mabingwa barani Ulaya.
Timu ya soka ya Juventus ya Italia imefanikiwa kusonga mbele katika hatua ya nusu fainali ya ligi ya mabingwa barani Ulaya baada ya usiku wa kuamkia leo kufanikiwa kutoka sare ya kutofungana na wenyeji wao Monaco ya Ufaransa.
Huu ulikuwa mchezo wa marudiano wa robo fainali ya ligi hiyo, baada ya mchezo wa awali uliochezwa nchini Italia wiki iliyopita, Juve kuifunga Monaco bao 1-0.
Juventus imefanikiwa kuingia hatua ya nusu fainali kwa faida ya ushindi wa mchezo wa awali.
Juventus imefanikiwa kuingia hatua hii ya nusu fainali toka mwaka 2003.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)







Hakuna maoni :
Chapisha Maoni