Wachezaji wa Paris Saint Germain ( PSG ) wakijifua katika uwanja wa Nou Camp jijini Barcelona nchini Hispania kabla ya mchezo wao wa marudiano na FC Barcelona leo usiku.
Ligi ya mabingwa barani Ulaya michezo ya marudiano robo fainali ya ligi hiyo itachezwa leo usiku katika viwanja viwili tofauti. Bayern Munich ambayo inasumbuliwa kwa kuwa na majeruhi, watakuwa nyumbani katika uwanja wa Allianz Arena kucheza na FC Porto toka Ureno.
Katika mchezo wa awali, Porto waliifunga Bayern mabao 3-1 na kujiweka pazuri katika mchezo wa leo kusonga mbele hatua ya nusu fainali ya ligi hiyo.
Wenyewe FC Barcelona ambao nao watakuwa katika uwanja wa nyumbani, wana nafasi nzuri ya kutinga hatua ya nusu fainali ya ligi hiyo baada ya mchezo wa awali kuwafunga PSG nyumbani kwao mabao 3-1.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni