Ijumaa, 24 Aprili 2015
NAIBU WAZIRI WA MAJI MHE. AMOS MAKALLA ATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAJI MUFINDI NA SONGEA
Naibu Waziri wa Maji,Mh Amos Makalla amefanya ziara ya kikazi wilaya ya Mufindi na Songea.
Akiwa wilayani Mufindi, Mh Makalla amekagua mradi mkubwa wa Maji wa ikilimanzoo na kuelekeza mkandarasi aukamilishe haraka.
Aidha Naibu Waziri huyo wa Maji amekagua na kutoa cheti kwa jumuiya ya watumia maji Mkongotema na Magingo (MAMKO).
Leo Ijumaa ataendelea na ziara yake wilaya ya Namtumbo kukagua miradi mbalimbali ya maji inayotekelezwa na serikali.
Naibu Waziri wa Maji Mh. Amos Makalla akimtwisha ndoo ya maji mwanafunzi wa darasa la sita katika shule ya Msingi Magingo.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)





Hakuna maoni :
Chapisha Maoni