.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 22 Aprili 2015

NANI KWENDA NUSU FAINALI LIGI YA MABINGWA ULAYA LEO, NI BINGWA MTETEZI REAL MADRID AU ATLETICO MADRID


Robo fainali ya ligi ya mabingwa barani Ulaya ukiwa ni mchezo wa marudiano utaunguruma leo katika viwanja viwili, lakini mchezo unaosubiriwa kwa hamu kubwa ni kati ya Real Madrid dhidi ya Atletico Madrid. 

Mchezo huo utakaochezwa katika uwanja wa Santiago Bernabeu unatarajiwa kuwa na upinzani mkubwa, kwani Real Madrid ambao ni mabingwa watetezi wa kombe hilo watakuwa na kibarua kigumu cha kuhakikisha hawavuliwi taji kwa kukubali kufungwa na Atletico hivyo kushindwa kufuzu kwa hatua ya nusu fainali ya ligi hiyo. 

Katika mchezo wa awali uliochezwa Vicente Calderon, timu hizo hazikufungana. 

Mchezo mwingine leo ni kati ya Juventus watakao kuwa ugenini kucheza na Monaco katika uwanja wa Stade Louis II nchini Ufaransa. Katika mchezo wa awali, Juventus waliichapa Monaco 1-0.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni