.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 29 Mei 2015

WAJUMBE 209 WA FIFA LEO WANATARAJIWA KUPIGA KURA

Wajumbe 209 wa mkutano mkuu wa Shirikisho la Soka Duniani Fifa leo wanatarajiwa kupiga kura ya kumchaguwa rais mpya wa Shirikisho hilo huko jijini Zurich, nchini Switzerland wakati shirikisho hilo linakabiliwa na kashfa nzito ya rushwa.

Rais wa shirikisho hilo la soka duniani Fifa Sepp Blatter anawania kuliongoza shirikisho hilo kwa muhula wa tano na anapambana na Prince Ali bin al-Hussein wa Jordan ambaye anawania nafasi hiyo.

Uchaguzi huo unafanyika siku mbili baada ya maafisa saba waandamizi wa shirikisho hilo kushikiliwa jijini Zurich katika uchunguzi wa tuhuma za kugushi unaofanywa na Serikali ya Marekani na kutaka watuhumiqwa hao kumi na nne kupelekwa nchini Marekani kufunguliwa mashitaka.

Blatter na Prince Ali wanatakuwa na muda wa dakika 15 kuhutubia mkutano mkuu wa baraza la shirikisho la soka duniani Fifa ambapo kila mjumbe kati ya wajumbe 209 wa mkutano huo ana haki ya kupiga kura katika uchaguzi huo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni