Meneja Kampeni wa Save the Children Internation, Jasminka Milovanovic, akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali Zanzibar kuhusiana na maadhimisho ya Siku ya Mtoto yanayotarajiwa kufanyika katika viwanja vya Amaan Zanzibar, mazungumzo hayo yamefanyika katika Wizara ya Wanawake na Watoto mwanakwerekwe Zanzibar
Mwanariadha Mkongwe wa Tanzania Suleiman Nyambui akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana ni mchezo wa riadha utakasowajumuisha watoto wa rika mbali katika sherehe za kuadhimishi Siku ya Mtoto inayotarajiwa kufanyika katika viwanja vya Amaan Zanzibar jumamosi kuazia asubuhi.
Miza Kona na Rahama Khamis Maelezo. 11/06/2015
Mimba za utotoni na mamba za umri mdogo ni madhara makubwa yanayopatikana kwa watoto wa kike ambazo hupelekea kukosa haki zake za msingi pamoja na kuishi katika maisha ya hatarishi.
Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Kazi na Utumishi wa Umma Mhe Haroun Ali Suleiman kwa niaba ya Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii, Vijana, Wanawake na watoto Bi Zainab Omar Moh’d wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari huko katika Ofisi hiyo Mwanakwerekwe.
Amesema kisheria mtoto chini ya miaka 18 ni kosa kumuozesha kufanya hivyo ni kumkosesha haki zake za msingi kwani mtoto bado anahitaji uangalizi wa wazee kwa kupata haki zake zote na kumlinda katika maisha yake.
“Madhara yanayopatikana kwa watoto wa kike wanaopata ujauzito pamoja na ndoa za umri mdogo ni kukosa haki zake za msingi, maisha yake kuwa hatarini kwa kujaribu kutoa ujauzito huo kwa njia zisio za kitaalamu kutokana na kuogopa aibu au kuogopa kufukuzwa majumbani na wazai wao”, amefahamisha Waziri Haroun.
Amefahamisha kuhsu madhara hayo ni kutoka damu nyingi wakati wa kujifungua na kupelekea kupoteza maisha pamoja madhara ya kukos elimu.
“Mara nyingi tumekuwa tukishuhudia kuwa ndoa za utotoni hazidumu hususan akiolewa na mtu mzima sana kwani mume huyo huona kuwa yeye ameoa tu na sio mlezi, kwani wakati huu mtoto huyu nahitaji kulelewa, kuelekezwa na kupata utulivu lakini ameoa hutajia mengi ambapo mtoto hana uelewa navyo na hatimae huamua kuachana na kupelekea madhara zaidi”, ameeleza Waziri huyo.
Aidha amekemea kutokomeza vitendo vya utelekeza wa watoto na udhalilishaji wa kijinsia ambavyo vinaendelea kuathiri jamii hivyo ameitaka jamii kutoa ushirikiano na kukubali kutoa ushahidi pale unapohitajika.
Waziri huyo ameeleza kuwa Wizara imeanzisha kituo cha huduma za simu kwa watoto “Child Help Line itakayotumiwa watoto, wanawake, vijana na jamii kwa jumla ambao wataweza kuripoti matukio ya udhalilishaji kwa njia ya simu na pia kupata msaada na ushauri nasaha ili kunusuru watoto na vitendo hivyo pamoja na kuwaunganisha na huduma nyengine pale inapohitajika.
Hata hivyo Mhe. Waziri amesema wizara anathamini juhudi na mshirikano ya Taasis za Kimataifa za Serikali na zisizo za Kiserikali katika masuala mbali mbali ya maendeleo ya watoto ambapo ujumbe wa mwaka hu ni
“TOKOMEZA MIMBA ZA UTOTONI NA NDOA ZA UMRI MDOGO”
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni