Mbunge wa Mvomero, Mh Amos Makalla akiongea wakati wa harambee ya kuchangia ujenzi wa Kanisa la Kigango cha Langali, Parokia ya Mgeta.
Mbunge wa Mvomero na Naibu Waziri wa Maji, Mh Amos Makalla leo ameongoza
Harambee ya kuchangia ujenzi wa Kanisa kigango cha Langali Parokia ya
Mgeta.
Katika harambee hiyo, jumla ya Fedha zilizopatikana ni shilingi milioni 12, na mgeni
rasmi Mhe mbunge wa jimbo la Mvomero Amos Makalla akichangia shilingi
milioni moja laki tano.
Aliwataka waumini na wananchi kujenga tabia ya kumtolea Mungu, kwani kila tulichonacho ni mali ya Mungu.
Amewawaeleza umuhimu wa waumini kujitoa kwa moyo ili kujenga kanisa
ambalo kitasaidia kufanya ibada kijijini hapo badala ya kwenda mbali
kijiji cha jirani.
Waumini waliojitokeza katika harambee hiyo.
Mbunge wa jimbo la Mvomero, Mh Amos Makalla akipokewa na waumini wakati alipofika kushiriki harambee ya kuchangia ujenzi wa Kanisa la Kigango cha Langali, Parokia ya Mgeta.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni