.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 16 Juni 2015

UN KUSAFISHA KILIMANJARO

FullSizeRender_1
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama akimkaribisha Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini Bw. Alvaro Rodriguez alipomtembelea kwa ajili ya mazungumzo.

Mratibu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania Bw. Alvaro Rodriguez, alikutana na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Bw. Leonidas Gama na kufanya naye mazungumzo.

Miongoni mwa mambo waliyojadili ni maandalizi ya shughuli na matukio kuadhimisha miaka 70 ya Umoja wa Mataifa (UN@70 ).
DSC_0046
Katika mazungumzo yao walikubaliana kufanya shughuli ya upandaji miti kuzunguka Mlima Kilimanjaro na kusafisha sehemu ya mji kabla ya Siku ya Umoja wa Mataifa.

Mkuu wa mkoa alikubaliana na wazo hilo na kusema shughuli hiyo inafaa kufanyika katikati ya mwezi wa Agosti.
FullSizeRender_3
                                                                      Wawili hao wakipiga picha ya pamoja.
FullSizeRender_4
                                                                                                                Wakiagana.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni