.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 27 Julai 2015

DAR WATAMBA MBIO ZA MAGARI ZILIZOFANYIKA ARUSHA

                                              Badhi ya magari yaliyoshiriki katika mashindano hayo

                                                               Na Woinde Shizza,libeneke la kaskazini blog

Mwendesha magari Randeep Shingh kutoka jijini Dar es Salam ameibuka mshindi katika mashindano ya kila mwaka ya mbio za nyika za magari nane-nane rally yaliyotimua vumbi katika mji wa Arusha mwishoni mwa wiki.

Mashindano hayo yamefanykia kwa siku mbili mfululizo huku yakishuhudiwa ushindani mkali kwa madereva hao waliotoka mikoa mbalimbali na Randeep Shingh akiwa na msoma ramani guvinder singh wa gari ya mistubish lancer akiibuka mshindi wa jumla katika mashindano hayo.

Katika mashindano hayo yaliyokuwa yakitofauti mwaka huu, baada ya kufungiwa mitambo ya kisasa ya kidigitali kwa kila gari ili kuwezesha ufuatiliwaji wa kila gari na njia zitakazopitia kwa ajili ya kuhakikisha kuwa hakuna zengwe wala suala la madereva kuiba njia na hata kupotea porini.

Zaidi ya madereva 20 kutoka ndani na nje ya nchi walioshindana zaidi ya Km 198 huku mshindi wa pili akiwa ni Raj Pal Dhani na msoma raman Sinder Sudle wakiwana na ghari la subaru impreza nafasi ya tatu ikiwa imeshikwa na Gurjit Singh .

Huku dereva mkongwe wa nchini tanzania Gerald Miller akiambulia nafasi ya sita, HUKU baadhi ya madereva walioshiriki katika mashindano hayo wakisema yalikuwa magumu mwaka huu huku wengine wakizungumzia changamoto ya barabara

Baadhi ya mashabiki wa mchezo waliojitokeza kwa wingi kutazama mashindano ya hayo ya utrack nanenane rally walisema wamefurahi na kuiomba serikali kuwezesha mashindano haya kufanyika mara kwa mara

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni