.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 27 Julai 2015

UWT WACHAGUA MADIWANI

Abbasi Mlanya Na yeremias ngerangera , Tunduru MKutano Mkuu wa jumuiya ya Wanawake Tanzania (Uwt) ya Chama cha mapinduzi WilayaninTunduru wamewachagua Madiwani wa Viti maalum waatakao shirikiana na wagombea wa udiwani katika kata zao.

Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo uliofanyika katika ukumbi wa Sky way Mjini hapa, mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM mkoa wa Ruvuma aliyeteuliwa kusimamia uchaguzi huo Bi.Awetu Matumla Akukweti alisema kuwa Tarafa ya Mlingoti washindi ni Bi. Siwema kalipungu na Atingala Mohamed.

Alisema katika matokeo hayo kalipungu alipata kura 380 kati ya kura 785 zilizo pigwa, Atingala alipata kura 371 na kuwabwaga wapinzani wao Bibie mandingo ambaye alipata kura 277, Fatuma kaisi kura 175, Rehema Machemba 121, Kanunu Mgomba 94, Pendo Luwambano 54 na Asha mpinga 17.

Alisema tarafa ya matemanga washindi ni Bi. Stawa Timamu alipata kura 799, Sharifa Niko 569 na kuwabwaga Ashura Rashid kura 179, Amina Mpepo 174,Aha Kihenge 158, na Amina Hokororo 153.

Kwa mujibu wa Akukweti, wajumbe hao waliwachagua Bi. Zenna Wina kwa kura 478 na Dani Malikuseka kura 453 kuwa wagombea wa nafasi hiyo katika tarafa ya Namasakata na kuwabwaga Bi awetu Ndeka kura 319 na Bi Rukia Makina aliyepata kura 187.

Katika tarafa ya Nalasi aliochaguliwa ni Aindi Daruweshi aliyepata kura 713 na Alusi Unusi kura 195 huku tarafa ya Lukumbule Alusi Ally akibuka kidedea kwa kupata kura 564 na Hadija kazibule kura 508 na kuwabwaga Bi. Habiba seph 338 na hadija Chipoka 226.

Kwa upande wa tarafa ya Nampungu wajumbe hao Bi. Rehema Nyoni alibuka mshindi kwa kura 602 huku akiwa anafuatiwa kwa na Bi.Hadija Napunda aliyepata kura 128 na tarafa ya Nakapanya Bi. Maimuna Bora aliibuka mshindi kwa kupata kura 576 na Fatuma Mapila 451 huku Hawa Machemba akishia kupata kura 308, Mwajuma Kalesi 154, Perepetua Makina 87,Dorini Tindo 78, Sofia Hasan 74, Mwanashungi Rashid 35
.
Awali akiongea na wajumbe hao katibu wa Uwt wilaya ya tunduru Bi. Fatuma Mandingo aliwataka wajumbe hao kutumia nafasi hiyo kwa umakini kwani endapo watafanya makosa kwa kuchagua wagombea wabovu adhabu yao ni miaka 5.

Alisema hata kama wamekwisha pewa fedha na baadhi ya wagombea hao, fedha hizo wale lakini wabakie na msimamo wao wa kuchagua Wagombea wenye uwezo na kuongea kuwa “ akilizakuambiwa, waongeze na zao” Mwisho

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni