.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 18 Agosti 2015

MAKALLA ATEMBELEA MIRADI YA MWAUWASA JIJINI MWANZA LEO

Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Amos Makalla akikagua mradi wa majisafi katika Kituo cha Majisafi cha Capri Point, akiwa pamoja na Mkurugenzi wa MWAUWASA, Inj. Anthony Sanga.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Amos Makalla akiwa kwenye mradi wa majitaka katika Kituo cha Kusukuma Majitaka cha Makongoro.
Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla na Msimamizi wa Ujenzi wa Jengo Jipya la MWAUWASA, Inj. Stanley Mwasawala (kushoto), ambalo ujenzi wake unaendelea katika eneo la Isamilo na unategemewa kukamilika Januari, 2016 pamoja na maafisa wengine waliombatana nae.

Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Amos Makalla akiambatana na Meneja Msaidizi wa Operesheni ya Tiba ya Maji (Sanitation Operation), Inj. Salim Lossindilo katika mradi wa tiba ya maji (sanitation) Butuja, unaopokea majitaka kutoka Makongoro na kuyatibu na kutumika kwa ajili ya matumizi mengine.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Amos Makalla akiwa pamoja na Bodi ya MWAUWASA, wafanyakazi wa MWAUWASA na maafisa wa Wizara ya Maji alipotembelea ofisi ya MWAUWASA, Capri Point.

Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Amos Makalla leo ameendelea na ziara yake Kanda ya Ziwa kwa kutembelea miradi ya Mamlaka ya Majisafi na Mazingira, jijini Mwanza (MWAUWASA) na kukagua utekelezaji na maendeleo ya miradi ya maji mkoani Mwanza.

Aidha, Mhe. Makalla aliweza kujionea ujenzi wa jengo jipya la MWAUWASA, Isamilo na kuzungumza na wafanyakazi wa MWAUWASA katika hafla fupi ya kuwazawadia wafanyakazi waliofanya kazi kwa uaminifu kwa zaidi ya miaka 15 katika ofisi za MWAUWASA zilizopo Capri Point.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni