Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Amos Makalla leo ameendelea na ziara yake Kanda ya Ziwa kwa kutembelea miradi ya Mamlaka ya Majisafi na Mazingira, jijini Mwanza (MWAUWASA) na kukagua utekelezaji na maendeleo ya miradi ya maji mkoani Mwanza.
Aidha, Mhe. Makalla aliweza kujionea ujenzi wa jengo jipya la MWAUWASA, Isamilo na kuzungumza na wafanyakazi wa MWAUWASA katika hafla fupi ya kuwazawadia wafanyakazi waliofanya kazi kwa uaminifu kwa zaidi ya miaka 15 katika ofisi za MWAUWASA zilizopo Capri Point.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni