Meya mmoja nchini Brazil ameingia
mitini baada ya kutuhumiwa kujichumia fedha za mfuko wa mfumo wa
shule na kuendesha mji anaouwakilisha kwa kutumia WhatsApp.
Meya huyo mwanamke Lidiane Leite,
25, anaishi maisha ya kifahari katika mji mkuu wa jimbo la Maranhao.
Imeelezwa kuwa Meya Leite alikuwa
akiwasiliana na mji aliochaguliwa kupitia mtu mmoja aliyejulikana
kama Bom Jardim, ambaye alikuwa akiwasilisha ujumbe kila siku wa
WhatsApp kwa baraza lake la madiwani.
Hati ya kukamatwa Meya huyo pamoja
na mwanaume wake ambaye inasemekana kuwa ndiye mshauri wake mkuu.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni