.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 21 Agosti 2015

MTU MWENYE SILAHA AMEMUUA MWANDISHI WA HABARI PETER JULIUS MOI NCHINI SUDANI KUSINI

Mtu mwenye silaha amemuua mwandishi wa habari Peter Julius Moi kwa kumpiga risasi mara mbili mgongoni katika Jiji la Juba, familia yake imethibitisha baada ya kutambua mwili wake.

Moi anakuwa mwandishi wa saba kuuwawa nchini Sudani Kusini kwa mwaka huu, wakati machafuko ya wao kwa wao yakiendelea.

Mauaji yake yametokea siku chache tu kupita tangu rais Salva Kiir kutishia kuua waandishi wa habari ambao wanaandika habari za kuikosoa serikali.

Hata hivyo msemaji wa rais amesema matamshi ya rais Kiir hayakueleweka vizuri, na polisi wameanza uchunguzi wa kifo cha Moi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni