Mwanaume mmoja huko
Chicago Marekani amepoteza nafasi ya kupata ajira baada ya kumtumia
kimakosa picha za utupu meneja uhusiano wa kampuni aliyoomba ajira.
Polisi wamesema
mwanaume huyo ambaye jina lake limehifadhiwa alituma picha za utupu
kati ya Agosti 11 na 13 kwa meneja uhusiano huyo mwanamke na baadae
kumpigia simu.
Meneja huyo mwanamke wa
kampuni mojawapo ya St Charles alipokea picha hizo zilizotumwa kama
ujumbe wa simu mara mbili akiwa nyumbani na kuwasiliana na polisi.
Msemaji wa polisi
amesema mwanaume huyo alikiri kutuma jumbe hizo lakini amesema picha
hizo alikuwa amelenga kumtumia mtu mwingine.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni